MICHEZO:WALLACE KARIA RAISI MPYA TFF

MICHEZO:WALLACE KARIA RAISI MPYA TFF

Timu nzima ya STAR SMART TV ONLINE ilipiga kambi kuhakikisha inapata matokeo ya uchaguzi wa Shirikisho la soka Tanzania.  Baada ya kusubiri kwa muda mrefu imefanikiwa kukuletea matokeo yote,
Rais mpya wa TFF ni Wallace Karia ambaye ameshinda kwa kura 95 kati ya na wajumbe waliopiga kura kwenye uchaguzi huo.




Matokeo ya uchaguzi mkuu wa viongozi wapya wa TFF yametangazwa rasmi mjini Dodoma baada ya zoezi zima la uchaguzi kukamilika.

Karia amewashinda Iman Madega, Shija Richard, Ally Mayay, Emanuel Kimbe na Fredrick Mwakalebela ambao walikuwa wakiwania nafasi ya urais wa TFF.
Kabla ya kuchaguliwa kuwa Rais wa TFF, Karia alikuwa makamu wa Rais chini ya Jamal Malinzi ambapo baadae aliendelea kuiongoza TFF baada ya Malinzi kuwa mahabusu akikabiliwa na mashitaka ya matumizi mabaya ya ofisi.
Karia ataongoza shirikisho la soka Tanzania kwa kipindi cha miaka minne kwa mujibu wa katiba ya TFF.
Nafasi ya Makamu wa Rais, Wambura alipata kura 85, alishindana na Mulamu Ngh'ambi aliyepata kura 25, Mtemi Ramadhan kura 14, Richard Selasela kura mbili.
Wajumbe wa kamati ya utendaji walioshinda kutoka katika Kanda 13 ni pamoja na  Kanda 13(Dar es Salaam) mshindi ni Lameck Nyambaya aliyepata kura 41. Kanda 12 (Kilimanjaro&Tanga) mshindi ni Khalid Abdallah aliyepata kura 70.
Kanda ya 11(Pwani&Morogoro) mshindi ni Francis Ndulane aliyepata kura 70, Kanda ya 10 (Dodoma&singida) mshindi ni Mohammed Aden aliyepata kura 35, Kanda ya 9 (Lindi&Mtwara) mshindi ni Dastan Mkundi amepata kura 74.
Kanda ya 8 (Njombe&ruvuma) mshindi ni James Mhagama aliyepata kura 60, Kanda ya 7 (Mbeya & Iringa) mshindi ni Elias Mwanjala aliyepata kura 61, Kanda ya 6 (Katavi&Rukwa) mshindi ni Kenneth Pesambili aliyepata kura 72
Kanda ya 5 (Kigoma&Tabora) mshindi ni Issah Bukuku aliyepata kura 80, Kanda ya 4  (Arusha&Manyara) Sarah Chao aliyepata kura 57, Kanda ya 3 (simiyu&shinyanga) mshindi Mbasha Matutu aliyepata 67, Kanda ya 2 (Mwanza&Mara) Vedastus Lufano alipata kura 67, Kanda ya 1 (Kagera&Geita) mshindi alikuwa Salum Chama alipata kura 90.                      
Ahadi 11 za Karia
Karia alizindua kampeni  na kutaja vipaumbele vyake 11 atakavyohakikisha anavisimamia kikamilifu.
Vipaumbele hivyo vilivyotajwa ni nidhamu ya muundo na mfumo, maendeleo ya vijana, wanawake na soka la ufukweni, mafunzo na ujenzi wa uwezo, mapato, uwezeshaji na nidhamu ya fedha, miundombinu na vifaa na maboresho ya bodi ya ligi.
Vingine ni ushirikiano wa wadau, udhamini na masoko, maboresho ya mashindano, uimarishaji mifumo ya kumbukumbu na ufanisi wa waamuzi.
Karia alisema kuwa atahakikisha vipaumbele hivyo vinafanyiwa kazi muda mfupi baada ya yeye kuingia madarakani.

0 comments :

 
Copyright © 2015. STAR SMART BLOG TZ
Blogger Templates